Mshahafu huo wa kale ambao umewashangaza wengi ulitunukiwa maktaba hiyo na raia wa Uturuki uliandikwa mwaka 1473 Miladia na mwanakaligrafia wa Kiislamu wakati huo Meliki El Esberi.
Msahafu huo uliandikw akwa kutumia mbinu ya kaligrafia ya Muhaqqaq badala ya ile ya Naskh ambayo ilikuwa inatumika kwa wingi wakati huo. Kwa sasa ni wataalamu tu wanaoweza kuuona msahafu huo kwa karibu huku wageni wanaotembelea maktaba hiyo wakipata idhini tu ya kuona nakala ya kidijitali.
Mkurugenzi wa Maktaba ya Nyaraka ya Ziya Bey, Dahiye Karagülle, anasema msahafu huo umeandikwa kwa njia maridadi yenye kumvutia kila anayeutazama.