IQNA

Magaidi wa Boko Haram watangaza utawala wa ‘Khilafa’ Gwoza, Nigeria

19:01 - August 26, 2014
Habari ID: 1443511
Wanamgambo wa kitakfiri wa kundi la Boko Haram wa nchini Nigeria wametangaza kuasisi kile walichokitaja kuwa ni utawala wa “Khilafa” huko kaskazini mashariki mwa mji wa Gwoza.

Abubakar Shekau  kiongozi wa kundi la Boko Haram amesema katika mkanda wa video wa dakika 52 kuwa, ameasisi utawala wa Kikhalifa katika mji wa Gwoza baada ya kuuteka mapema mwezi huu.
Shekau ameongeza kuwa yeye na wanamgambo wa kundi la Boko Haram wamekuja kuishi katika mji huo na kwamba hawakusudii kuondoka katika mji huo.
Hata hivyo jeshi la Nigeria kwa upande wake limepingag madai ya kiongozi huyo wa Boko Haram juu ya kuuteka mji wa Gwoza.
Boko Haram ni kundi lenye misimamo ya kufurutu mipaka nchini Nigeria ambalo kutokana na kuwa na ufahamu mbaya na potofu kuhusiana na Uislamu, limeitumbukiza nchi hiyo katika dimbwi la machafuko na mauaji sambamba na kuzusha hitilafu za kidini na kikabila nchini humo.
1443021

Kishikizo: BOKO HARAM shekau potofu
captcha